Skip to main content

SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI (CERVICAL CANCER)


Saratani ya Shingo ya Kizazi (cervical cancer)yasemekana kuwa yaongoza kwa kusababisha vifo vya  wanawake nchini Tanzania

Kati ya wanawake 6,210 waliopata nafasi ya kugundulika kwa ugojwa huu 4,355 wasemekana kufariki dunia.  
(Imaworldhealth, 2010)




Saratani ya shingo ya kizazi ni ugonjwa ambao hutokana na mabadiliko ya mfumo wa  chembe zilizoko  katika shingo ya kizazi, kubadilika zikishamiri na kuzaliana kwa kasi kinyume na mpangilio wa kimaumbile na hivyo kupelekea ongezeko la upatikanaji wa saratani.



NINI KISABABISHACHO SARATANI YA SHINGO YA UZAZI ?


Utafiti wa kisayansi umeafiki kwamba 99%  ya saratani za shingo ya uzazi hutokana na maambukizi ya virusi vya 'Human Papillomavirus' (HPV).

Virusi hivi vilivyoko katika jamii ya papilloma vina aina zaidi ya 100,ambazo baadhi yake huambukizwa kwa njia ya  kujamiana.





BAADHI YA MAMBO YANAYOONGEZA  HATARI  ZA KUPATA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI?
  • Kushiriki tendo ndoa katika  umri mdogo au chini ya miaka 18
  • Kuwa na wenzi tofauti au mwenzi aliye na wapenzi tofauti
  • Utumiaji wa sigara kwani hupunguza nguvu ya kinga mwilini(impairs immune system)
  • Watu wenye kinga hafifu ya mwili au magojwa kama Ukimwi
  • Uzazi wa mara kwa mara

BAADHI YA DALILI ZA SARATANI YA KIZAZI
  • Kutokwa na majimaji au uchafu wenye harufu kali ukeni.
  • Kutokwa na damu ukeni mbali na siku za mwezi au baada ya tendo la ndoa
  • Maumivu makali ya sehemu ya chini ya tumbo ( pelvic area)
  • Kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiiana.
  • Kupungua kwa uzito wa mwili bila kukusudia
  • Mkojo wenye matone ya damu

PAP TEST (PAPANICOLAOUS TEST)

Pap-Smear ni test ambayo hutumika  kuchunguza  mabadiliko ya chembe zilizopo katika mlango wa kizazi  (cervix) ili kugundua mabadiliko yanayotokea katika chembe hizo mapema na hivyo kuyakabili mapema, kwani Saratani ya shingo ya kizazi yaweza kutibika iwapo itagundulika mapema.

Test hii hushauriwa kwa wanamke wa umri wa miaka 21 hadi 65  na chini ya umri wa miaka 21 endapo umeingia katika tendo la ndoa kwa kipindi cha kisichopungua miaka 3.




KUPUNGUZA HATARI ZA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI?

  • Pap tests.  Pata test hii mara kwa mara kuanzia mwaka 1 hadi 3,hii itategemea ushauri wa daktari wako,umri na majibu uliyoyapata ili kugundua chembe zisizo sahihi mapema na kuwahisha tiba.

  • Get an HPV vaccine (hii yashauriwa kati ya umri wa miaka 12 hadi 26.

  • Kuwa na mpenzi mmoja. Kitendo cha kuwa na mahusiano ya kimwili na mtu mmoja hupunguza hatari za maambukizi ya magojwa ya zinaa.

  • Tumia kinga (condoms). Hii husaidia kupunguza maambukizi ya magojwa ya  zinaa  


Shukrani/Thanks;

Ignatavicius, D.D. & Workman, M.L. (2010). Medical-Surgical Nursing: Patient-Centered Collaborative Care (6th ed.).
(WHO/ICO HPV Information Centre 2010)
https://www.imaworldhealth.org/archive/cervical
(WHO/ICO HPV Information Centre 2010)

Comments

  1. niligunduliwa na saratani mnamo 2019 na nimekuwa nikitafuta tiba tangu wakati huo. Oktoba mwaka jana nilipokaribia kukata tamaa, nilikutana na chapisho kwenye mtandao ambapo nilinakili barua pepe ya mwanamume anayeitwa dr DAWN inayotoa suluhisho la mitishamba kwa magonjwa. niliwasiliana naye na kupata maelewano naye akanitumia dawa ya mitishamba kupitia united parcel service pamoja na maelekezo ya jinsi ya kuitumia. kwa mshangao wangu mkubwa, nilipona baada ya siku 14 za kutumia dawa kama alivyohakikishiwa na daktari.
    Niliamua kushiriki hii kwa sababu najua kuwa kuna watu wengi huko ambao wanahitaji msaada. au umtumie ujumbe kwa WhatsApp.+2349046229159 Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

    Anaweza pia kuponya magonjwa mengi kama hayo

    {1}VVU na UKIMWI

    {2}Kisukari

    {3}Kifafa

    {4} Saratani ya Damu

    {5} HPV

    {6} ALS

    ReplyDelete
  2. "Niligunduliwa na saratani ya hatua ya 4 na nikapewa miezi ya kuishi. Kwa kukata tamaa, niligeuka kwa Dk. Dawn, ambaye mpango wake wa matibabu wa ubunifu na usaidizi usio na shaka ulibadilisha kila kitu. Ndani ya wiki, nilihisi kuwa na nguvu zaidi, na baada ya miezi ya huduma yake, uchunguzi wangu haukuonyesha athari ya kansa. Utaalamu na huruma ya Dk. Dawn ilinipa maisha yangu nyuma-nina uthibitisho hai wa kazi yake ya muujiza!"
    Ninapendekeza Dr Dawn kwa mtu yeyote anayepambana na saratani, UKIMWI, herpes na kadhalika, tuma barua pepe, dawnacuna314@gmail.com
    Whatsapp: +2349046229159

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili...

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwang...

.KUKABWA NA JINAMIZI A.K.A "SLEEP APNEA"

Je unahisi dalili zifuatazo? Kukoroma  kwa sauti kubwa hata kusumbua  mwenzio Uchovu unapoamka japo umelala usiku kucha  Maumivu ya kichwa unapoamka Mdomo au koo kuwa kavu unapoamka  Kusimamisha pumzi usingizini Kuzinduka mara kwa mara usingizini ukitafuta pumzi, kukabwa au kukohoa.? Usingizi wa mara kwa mara unaoingiliana na kazi,masomo,usalama barabarini. Ugumu wa kukaa macho kwa mda wakati wa vikao, kujisomea au kutazama TV Dalili kubwa ya Sleep Apnea ni kukoroma kwa sauti ya kuzidia na hata kukera mwezio Pict.Courtesy  of http://always-healthy.com/sleep-apnea  Harvard School of Medicine  yatoa ufafanuzi zaidi kuhusu ‘Kukabwa na Jinamizi’ a.k.a 'Obstructive Sleep Apnea'  (Ukosefu wa pumzi Usingizini) Video courtesy of Harvard School of Medicine UFAFANUZI NA ATHARI ZA UKOSEFU WA PUMZI USINGIZINI Binadamu yeyote anaposinzia mwili hulegea na viungo hupumzika.Ulegevu...