Skip to main content

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0








Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi .
Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye.

Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo
mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba.

Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha.


DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia)

Kipimo cha sukari  chini ya   70 mg/dL au 3.9 mmol/L  
chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ;
  • Njaa
  • kuumwa kwa kichwa
  • Kutokwa kwa jasho
  • kutikisika kwa mwili
  • Hasira
  • Mwili au ngozi baridi na nyevu
  • Kizunguzungu
  • Mapigo  kasi ya moyo
  • Kushuka kwa pressure ya damu
  • Kutoa sauti kubwa au kulia endapo yu usingizini
  • Uhafifu wa kuona
  • Upungufu wa ufahamu ( kuchanganyikiwa )au kusema vitu visivyoeleweka
  • Ugumu wa kuongea
  • Kuzimia

TIBA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)


Kinywaji au kitafunio hutumika kwa usalama kwa wale wanye fahamu na kuweza kumeza, kwa waliopoteza fahamu wahitaji kupata msaada wa haraka kwa mtaalamu



Serving Size (15 grams)
Carbohydrate Food
1/2 cup
Regular soda pop/
1 cup
Skim or 1% milk
1/2 cup
Fruit juice
3-4
Glucose tablets
4 teaspoons
Sugar
1 Tablespoon
Honey, syrup, or jam
5-6
Hard candies (i.e. Lifesavers or peppermints)
Baada ya treatment hii subiri  kwa dakika 15 na pima sukari ambayo inatakiwa kuwa kati ya  70-110 mg/dl  au 3.9 - 6.2 mmol/LKwa kipimo kilicho chini zaidi,  waweza kurudia treatment hii hadi mara tatu na kupima tena sukari, kama bado kipimo cha ashiria sukari iliyo chini pata msaada wa haraka na kumwona daktari au call 911..






The 15:15 rule holds that 15 grams of sugar followed by a wait of 15 minutes will return low blood sugar to normal levels

UPUGUFU WA SUKARI MWILINI KWA WAGONJWA WA KISUKARI WAWEZA KUSABABISHWA NA ;

  1. Insulin complications
  2. Kupitiliza saa za  mlo na ukosefu wa chakula
  3. Utumiaji wa pombe 
  4. Baadhi ya dawa ( eg. quinine,....)
  5. Kwa wale wenye diabetes Type 1 ni  muhimu sana kupima na kutumia kitafunio kabla ya mazoezi, kwani mazoezi ya mda mrefu yaweza kukuweka kwenye hatari ya upungufu wa sukari mwilini.


Insulin  ni hormone ambayo huzalishwa na chembe za  kingosho(pancreas)  pale ambapo umekula au sukari iko  juu kwenye damu.Hivyo insulin husisimua chembe za mwili kunyonya sukari  na kuhifadhi kama mafuta au nguvu ya akiba  huku ikibakisha kiwango cha kutosha katika mzunguko wa damu. (kwa wale wenye ugojwa wa sukari  umbile hili halifanyi kazi  vizuri   na hivyo yabidi kutegemea insulin ya bandia ili kuweza simamia(kucontrol)  kiwango cha sukari kwenye mzunguko wa damu )


Na vile vile Kingosho hichi, husisimua uzalishaji wa glucagon ambayo ni kama chakula,nguvu au sukari pale upungufu unapotokea; kwa mfano wakati wa njaa,mafungo au kupungukiwa na sukari kwenye damu. Hivyo sukari au glucose huongezeka katika mzunguko wa damu.


Tatizo ni pale tunapochanganya haya mawili, kwani wengi wamepoteza maisha kwa kuwekewa  Insulin pale wanapoonyesha dalili za kuishiwa na sukari mwilini. Insulin siyo ya mtu aliyehishiwa sukari kwani insulin huzidi kunyonya sukari kutoka kwenye damu  na kutuweka katika hifadhi ya mwili,hivyo damu inakaukiwa sukari na kumweka mgojwa kwenye  hatari ya kuishiwa nguvu,kupoteza ufahamu au kuzimia na pale isipopata suluhishi coma hata kifo hutokea. Mtu aliyeishiwa sukari anahitaji kuongezewa kama maelezo yaliyotangulia na pale anapokuwa amepoteza ufahamu na kushidwa kunywa au kula kitafunio, mtaalamu wake hutoa sindano ya glucagon ya kuongeza sukari mwilini .



Ushauri kwa wagojwa wa kisukari 



  1. Kuvaa bangili inayoashiria tatizo lako yaweza kukusaidia, kwani itatoa ufafanuzi zaidi kuhusu  cha kufanya au kuepuka kufanya endapo umepoteza fahamu.
  2. Ni vizuri kutembea na kitafunio au kuweka glucose,pipi,hasali au juice katika office au nyumbani kwani huwezi jua ni lini itahitajika kwa haraka.
  3. Ni vyema kukaa chini  na familia yako na mufunzane kuhusu ugojwa huu   na namna ya kukabiliana nao, kwani huwezi jua lini na ni wapi itatokea.
  4. Fuata masharti ya daktari wako; epuka mikate, nyama nyekundu,mikaango,  wali mweupe na pombe, kwani vyazidi kukuumiza.
  5. Tumia brown rice(ile yenye makapi yake, loeka kabla ya kupika), kunde,oatmeal na mboga za majani (hasa salads husaidia kunyonya  sukari mwilini).
  6. Pata mazoezi ya kutembea kila siku ,hii husaidia sana kupunguza sukari katika mzunguko wa damu bila kuihifandhi mwilini na kuongeza uzito,kurahisisha mzunguko wa damu mwilini,kupunguza ongezeko la cholesterol na kudumisha umahiri wa vishipa kwani hili ni tatizo kubwa kwa wagojwa wa kisukari na ndio maana wengi huwa na matatizo ya vidonda visivyopona. 
  7. Kagua miguu na vidole mara kwa mara, kwani wengi wenye kisukari,hupoteza hisia ya sehemu mbali mbali mwilini na kutojua kama wanakidonda. Hii yaweza chelewesha huduma ya haraka na kusababisha kidonda sugu na infection ambacho mara nyingi ndio chanzo cha kukatwa kwa kiungo hicho.  
  8. Epuka viatu vya kubana na kuchubua ngozi
  9. Kata kucha mara kwa mara na hakikisha usafi wake.
  10. Pima wa joto la maji kabla ya kuogea. Ugojwa wa kisukari una hatua tofauti na pale unapodhuru mishipa ya mwili (diabetic neuropathy) mgojwa anaweza kuwa anaunguwa na maji ya mot bila kuhisi maumivu na hivyo kuwa kwenye matatizo makubwa.  


.


I



Shukrani;
Ignatavicius, D.D. & Workman, M.L. (2010). Medical-Surgical Nursing: Patient-Centered Collaborative Care (6th ed.). Philadelphia: Elsevier/Saunders.
www.webmd.com/a-to-z.../symptoms-of-low-blood-sugar-topic-overvie

Comments

Popular posts from this blog

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko