Skip to main content

UKITUNZA MIFUPA UTASAIDIKA UZEENI !


Osteoporosis ni ugojwa sugu  wa  mwili kujitafunia virutubisho vilivyo kwenye mifupa na kuvitumia kwa mahitaji  yake.Hii husababisha  upungua wa umahiri wa  mifupa(bone density)  kuifanya iwe hafifu na  kumegeka. Ugojwa huu huitwa  “ silent disease’ kwani mara nyingi hujulikana tu  pale mtu anapoanguka na kuvunjika (kwa urahisi sana au kupata  fructure)   tofauti na mtu asiye na tatizo hili. 

UNDANI MDOGO KUHUSU  OSTEOPEROSIS



                                                                                                                      Mifupa ya mwili kwa wakati wote huwa  na mabadiliko ya  kujingeka, kujiimarisha   na
kujirepea(bone remodeling) kwa kupitia mzunguko maalaum wa kusagika(osteoclast) ambapo hutoa madini yake ya calcium  katika mzunguko wa damu. Osteoperosis na upungufu wa umahiri wa mifupa (low bone mass)hutokea pale ambapo usagikaji wa mifupa (Osteoclast) uko juu zaidi ya  ujengekaji wa mifupa (Osteoblast).
Binadamu hufikia kilele cha ujenzi  wa mifupa kati ya umri wa miaka 25 -30,kwani kabla ya umri huu mifupa hujijenga zaidi na kusagika kwa kiwango kidogo kama inavyotakiwa.Baada ya umri wa miaka 30,usagikaji wa mifupa huuzidia kwa kina kikubwa kuliko ujengakaji wa mifupa.Hivyo upelekea upungufu wa umahiri wa mifupa( decrease bone density ).

Hii inatuonyeesha jinsi gani madini ya calcium ni muhimu mwilini kwani ulaji wa chakula kisichojumuisha calcium na vitamin D (vitamin D husadia unyonyaji wa madini ya calcium kutoka kwenye chakula) husababisha mwili kutumia calcium iliyohifadhika katika mifupa. Ili  calcium iweze kujitoa katika mifupa (hifadhi yake) na kutumika mwilini(ktk mzunguko wa damu), yabidi mifupa ipitie hatua ya kujisaga na kutoa kirutubisho hicho kinachohitajika na  hivyo kutuacha na mifupa hafifu.


Japo  Osteoperosis imekuwa ikiwapata zaidi wanawake waliyomaliza siku za mwezi (post menopausal Women) au umri wa miaka 50 na kuendelea.Leo tunaona kina dada/kaka wadogo ambao wanatunza miili yao kwa kuinyima virutubisho wakihathirika kwani umri ufikapo miaka 30, mwili unatumia hifadhi zake zaidi ya kuwekeza na hivyo hujikuta katika hatari za osteoporosis.


VIJANA WALIO HATARINI KUPATA OSTEOPEROSIS;

  • Wanawake kwa wanaume wanaoingia kwenye diet kali za kupunguza mwili na kukosa viritubisho vya kutosha wakati mifupa bado inajijenga .Kwani umri chini ya miaka 25-30 bado  una uwezo wa kuhifadhi calcium kwenye mifupa na kuifanya imara. Iwapo umri huu kumekuwa na upungufu wa madini haya  mifupa  huwa ni hafifu na kuzidia pale umri unapoongezeka.
  • Kundi lingine haswa ni kwa wale wenye matatizo la  kula mfano;  anorexia nervosa  au wanao kula na kujitapisha ili kuzuia ongezeko la mwili (bulimia)



Japo wapo ambao wanaona  ni rahisi kumeza kidonge cha Calcium,vidonge hivi vinaweza kukudhuru na zinahitaji maelezo na ushauri wa daktari.vidonge vya calcium vyaweza kusababisha mawe  kwenye figo na matatizo ya moyo hasa pale vinapotumika bila mpangilio .

RISK ZA OSTEOPOROSIS NI PAMOJA NA ;
  • Miaka 65 au zaidi  kwa mwanawake
  • Miaka 75 na zaidi kwa wanaume
  • Historia kifamlia
  • Wanawake waliomaliza kupata siku za mwezi
  • Mwili mdogo au mwembamba sana(hasa wazungu wenye mifupa midogo)
  • Upungufu wa Calcium
  • Utumiaji wa sigara
  • Utumiaji wa pombe kwa wingi
  • Ukosefu wa mazoezi ya mwili
  • Kutotembea kwa mda mrefu kwa wale walio kitandani(bed ridden)
  • historia ya kuvunjika baadaya miaka 50 
  • Baadhi ya dawa kama steroids. na magojwa tofauti kama diabetes,hyperthyroidism,bone cancer.... 
DALILI ZIJULIKANAZO NI PAMOJA NA ;
  • Maumivu ya mgongo au tenderness,stiffiness
  • Maumivu ya  kiganja cha mkono  wakati wa kubeba mzigo 
  • Maumivu ya mgongo unapojeuka au kuinama
  • Maumivu yanayozidia na shughuli na kupungua ukipumzika
  • Ugumu wa viungo wakati wa kuamka au maumivu
  • Kuanguka na kuvunjika(hii uhashiria mifupa iliyodhoofuka) 
MATUNZO YANAYOSHAURIWA KWA MIFUPA YA MWILI

  • Pata mazoezi ya kutembea walau dakika 30 mara 3 - 5  kwa wiki kwani hupunguza chances za kupata osteoperosis.
  • Hakikisha unapata calcium kama kutoka kwenye  maziwa na mboga za rangi nzito ya kijani
  • Kupata mwanga wa asubuhi wa jua ambao ni vitamin D kwani vitamin D ni muhimu sana mwilini na huwezesha unyonyaji wa calcium kutoka kwenye chakula na kuiweka katika mzunguko wa damu na hifadhi katika mifupa.
  • Mazoezi  laini ya vyuma  (weight bearing  exercises) yasemekana hupunguza usagikaji wa mifupa na kusisimua ujengekaji wa mifupa.
  • Epuka utumiaji wa caffeine au vinywaji vyenye carbon kama soda nk. kwani huchangia kuondoa calcium mwilini kupitia mkojo na hivyo kuweka mwili  katika ongezeko la hitaji ya calcium.
  • Punguza utumiaji wa pombe na epuka  sigara kwani vyote hupunguza umahiri wa  mifupa kujijenga

  • Utumiaji wa vyakula vya protein kwa kiwango kizuri husaidia ufanisi wa calcium mwilini kwani calcium huhitaji mazingira yenye protein ili kufanya kazi yake kimahiri.
  • Pia kuwa mwangalifu kwani “high protein diet” hutuweka katika hatari za upungufu wa calcium kwani protien ikizidi sana huchangia kutoa calcium mwilini kupitia mkojo.


"Protein;Kiwango cha protein kwa mtu mzima ni  0.8 grams/Kg kwa siku. Protein ni muhimu kwa afya ya mifupa haswa katika kuponyesha majeraha na mifupa iliyovunjika na hata vidonda mwilini. 


SHUKRANI/THANKS;

Ignatavicius, D.D. & Workman, M.L. (2010). Medical-Surgical Nursing: Patient-Centered Collaborative Care (6th ed.). Philadelphia: Elsevier/Saunders.
magina65.blogspot.com - Images
| 


Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko