Skip to main content

TATIZO LA ALLERGY LAWEZA TISHIA USALAMA.


Mchezaji wa Cinema Will Smith katika movie ya Hitch akionyesha ukweli wa allergy za vyakula

Wengi wenye allergy za vyakula hasa karanga hugundua hata pale  wanaposikia harufu kwani macho yaanza kutoa machozi au wanapiga chafya. Mbaya zaidi ni pale  wanapotumia  vyakula vyenye mchanganyiko wa karanga kwani hali zao huwa ni mbaya na uhitaji matibabu ya haraka. Allergy ya chakula kilichoingia mwilini  huweka mwili  mzima katika  hatari kwani mwili mzima huingia katika kujibu mashambulizi ya kile kisichokubalika mwilini kwa dalili zifuatazo;



BAADHI YA  DALILI ZA (ANAPHYLAXIS) ALLERGY MBAYA INAYOHUSIHA 

MWILI MZIMA NA KUHATARISHA MAISHA;

  • Vipele vya harara mwilini,kuwashwa,kuwa mwekundu
  • Mafua ya ghafla ya maji
  • Kuvimba kwa mwili
  • Kupumua kwa shida na kukohoa
  • Ugumu wa kuongea
  • Kuumwa tumbo
  • Kizunguzungu
  • Kuhisi kitu kibaya kitakotea au wasiwasi mkubwa
  • Kuvimba mwili,nje na ndani na hasa njia ya hewa na kusababisha kushidwa kupumua
  • Ongezeko la mapigo ya moyo
  • Kushuka kwa pressure ya damu na kupoteza fahamu
  • kichefuchefu,kutapika au kuarisha
Dalili hizi zisipokabiliwa kwa haraka huweka mwili kwenye hatari kubwa kwani mwili huvimba na hata kufunga njia ya hewa . Wengi wenye allergy mbaya wapatapo dalili hizi hutumia Epipen ambayo ni prescripiton kutoka kwa daktari inayosadia kupunguza na kuzuia shock ya mwili,kusimamia pressure ya damu na kupunguza kubanwa kwa njia ya hewa na kuruhusu mapafu kuruhusu pumzi pale ambapo allergy inaongeza uvimbe, kufunga njia hiyo na mwishowe kuweka mwili kwenye shock.

KWA WATOTO WENYE ALLERGY HII NI MUHIMU:
  • Kumfundisha mtoto kuhusu allergy yake
  • Kutomruhusu  mtoto kulishwa au kula chakula usichokijua  viungo vyake
  • Kutembea na dawa zake kwa wakati wote
  • Kujua namna ya kutumia dawa zake endapo anajikuta mbali na msaada wako
  • Ni vyema wote kama familia mnaweka jitihada za kuepuka vyakula hivyo ndani ya nyumba na kufunza kila mmoja wenu namna ya kutoa huduma ya haraka kutokana na ushauri wa daktari.

BAADHI YA DAWA ZITUMIKAZO;
Benadrly na Epi-Penn -kwa maelezo kamilifu ongea na DAKTARI wako


Shukrani;
http://gotmymoxie.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko