Skip to main content

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM
Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit)


Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama;

Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu.Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa Hyperkalemia au ongezeko la potassium katika damu.
Kiwango cha potassium kikizidi mwilini au kupunguwa ni hatari kwa usalama kwani huleta hitilafu katika mapigo na utendaji wa moyo na hivyo huhitaji maangalizi ya haraka.



Ni kinachoweza sababisha Upungufu wa Pottasium Mwilini ? ( Hypokalemia)

Hali hii huweza tokea pale mwili unapopoteza chumvi chumvi mwilini hasa kwa njia zifuatazo;


  • Kuharisha ,
  • Kutapika,
  • Kutokwa jasho kwa wingi kupita kiasi
  • Baadhi ya dawa za magojwa ya moyo na shinikizo la damu hasa za kupunguza maji mwilini kupitia njia ya mkojo, kama Loop Diuretics
  • Matumizi ya kuzidia ya dawa au mitishamba ya kusaidia upatikanaji wa haja ( laxatives)


Dalili za Upungufu wa Potassium mwilini

  • Kuumwa kwa misuli na kuhisi uchovu wa misuli (muscle cramps and weakness)
  • Uchovu
  • Kuvurugika kwa tumbo
  • Mapigo ya moyo yenye hitilafu katika vipimo
  • Upungufu wa chumvi mwilini
  • Usingizi wa mara kwa mara
  • Hasira
  • Uhafifu wa utendaji wa figo
  • Upungufu wa umahiri wa moyo
  • Kupungukiwa na kumbukumbu
  • Na hata kifo pale kiwango kinapokuwa chini sana kwani moyo hushidwa kuendeleza mapigo sahihi.


Ongezeko la ziada la Potassium mwilini (Hyperkalemia)

Hali hii husababisha mapigo ya moyo yenye hitilafu na ni  hatari kwa maisha na huweza sababishwa na ;


  • Dawa za magojwa ya moyo zilizopo kwenye kundi la ACE inhibitor na  Potassium Sparing Diuretics
  • Maambukizi
  • Hitilafu katika utendaji wa figo
BAADHI YA VYAKULA VYENYE MADINI YA POTASSIUM


w








Na vingine vingi ……………..

Shukrani;

http://umm.edu/health/medical/altmed/supplement/potassium
 Potter, P.A. & Perry, A.G. (2009)

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko