Skip to main content

UVUTAJI SIGARA HAUNA TOFAUTI NA UNYWAJI SUMU WA TARATIBU !.








        MAPAFU YA  ASIYEVUTA SIGARA                                 NA                                          MVUTA SIGARA 
  
Uvutaji wa sigara na mazingira yaliyokuwa na moshi wa sigara ( second hand smoke) hujulikana kwa  maafa yake ya husababisha magonjwa sugu ya mapafu yajulikanayo kama  ‘Chronic Obstructive Pulmonary Diseases” (COPD) yakiwemo pumu, kifua kikuu na …?(emphysema). Magonjwa haya uhashiriwa na upungufu wa umahiri wa ubadilishaji wa hewa katika mapafu; ugumu wa kutoa  hewa chafu ya carbon katika mapafu  na uchukuaji wa hewa oxygen. Hii hujitokeza pale mgonjwa anapojihisi ugumu wa kuvuta hewa hasa wakati wa shughuli au mazoezi.















Mbali na magojwa sugu ya mapafu,uvutaji wa sigara watupelekea saratani za aina mabalimbali kama :-

  • Saratani ya mapafu
  • Saratani ya njia ya chakula (umio au esophagus) 
  • Utumbo, 
  • Njia ya kutolea uchafu mwilini,
  • Ini,figo na njia ya mkojo 
  • Kigosho, tumbo na  koromeo.



Uvutaji wa sigara waweza kupunguza uwezo wa uzazi kwa mwanamke kuharibu afya ya mtoto kabla  ya kuzaliwa pamoja na ;
  • Kuzaliwa kwa mtoto ambaye hajatimia siku za kuzaliwa(premature)
  • Kufariki kwa mtoto kabla ya kuzaliwa (stillbirth)
  • Mtoto mwenye uzito mdogo au chini ya kipimo wakati wa kuzaliwa
  • Kifo cha ghafla kwa mtoto mchanga ( sudden infant death syndrome; SIDS)
  • Mimba iliyojipachika nje ya kizazi (Ectopic pregnancy)
  • Mtoto mwenye hitilafu sehemu za midomo 
ZITAKAPO MDOMO (CLEF LIP )
UZITO PUNGUFU WAKATI WA KUZALIWA ( Low birthweight <5.5 pounds)


Uvutaji sigara huchangia kuharibu  mbegu za kiume na kupunguza nguvu ya uzazi pamoja na kupelekea hitilafu za kuzaliwa na upoteaji wa mimba changa.Wanawake wanaovuta sigara waliopita umri wa uzazi wana ongezeko la uhafifu wa mifupa hivyo huvunjika kwa urahisi pamoja na afya duni  ya meno na fizi.Uvutaji wa sigara wasemekana kwa kupelekea  hatari zaidi ya  kupata stoke na  magonjwa ya moyo mara 2 hadi 4 na upofukaji wa macho ukilinganisha na mtu asiye mvutaji wa sigara pamoja na Burgeres disease ‘ugojwa ambao unaathiri mishipa ya damu ya mikono na miguu.
BURGERS DISEASE



Shukrani: Thanks
http://ahealthylifefitness.blogspot.com/
DR M.A. ANSARY/SCIENCE PHOTO LIBRARY
http://www.cdc.gov/tobacco/campaign
funmasti1.blogspot.com
www.kaskus.co.id - 34Burgers Disease
article.wn.com 
aboutbabyarticle.blogspot.com 
http://www.ncbi.nlm.nih.gov/pubmed/2644816

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko