Skip to main content

SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI (CERVICAL CANCER)


Saratani ya Shingo ya Kizazi (cervical cancer)yasemekana kuwa yaongoza kwa kusababisha vifo vya  wanawake nchini Tanzania

Kati ya wanawake 6,210 waliopata nafasi ya kugundulika kwa ugojwa huu 4,355 wasemekana kufariki dunia.  
(Imaworldhealth, 2010)




Saratani ya shingo ya kizazi ni ugonjwa ambao hutokana na mabadiliko ya mfumo wa  chembe zilizoko  katika shingo ya kizazi, kubadilika zikishamiri na kuzaliana kwa kasi kinyume na mpangilio wa kimaumbile na hivyo kupelekea ongezeko la upatikanaji wa saratani.



NINI KISABABISHACHO SARATANI YA SHINGO YA UZAZI ?


Utafiti wa kisayansi umeafiki kwamba 99%  ya saratani za shingo ya uzazi hutokana na maambukizi ya virusi vya 'Human Papillomavirus' (HPV).

Virusi hivi vilivyoko katika jamii ya papilloma vina aina zaidi ya 100,ambazo baadhi yake huambukizwa kwa njia ya  kujamiana.





BAADHI YA MAMBO YANAYOONGEZA  HATARI  ZA KUPATA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI?
  • Kushiriki tendo ndoa katika  umri mdogo au chini ya miaka 18
  • Kuwa na wenzi tofauti au mwenzi aliye na wapenzi tofauti
  • Utumiaji wa sigara kwani hupunguza nguvu ya kinga mwilini(impairs immune system)
  • Watu wenye kinga hafifu ya mwili au magojwa kama Ukimwi
  • Uzazi wa mara kwa mara

BAADHI YA DALILI ZA SARATANI YA KIZAZI
  • Kutokwa na majimaji au uchafu wenye harufu kali ukeni.
  • Kutokwa na damu ukeni mbali na siku za mwezi au baada ya tendo la ndoa
  • Maumivu makali ya sehemu ya chini ya tumbo ( pelvic area)
  • Kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiiana.
  • Kupungua kwa uzito wa mwili bila kukusudia
  • Mkojo wenye matone ya damu

PAP TEST (PAPANICOLAOUS TEST)

Pap-Smear ni test ambayo hutumika  kuchunguza  mabadiliko ya chembe zilizopo katika mlango wa kizazi  (cervix) ili kugundua mabadiliko yanayotokea katika chembe hizo mapema na hivyo kuyakabili mapema, kwani Saratani ya shingo ya kizazi yaweza kutibika iwapo itagundulika mapema.

Test hii hushauriwa kwa wanamke wa umri wa miaka 21 hadi 65  na chini ya umri wa miaka 21 endapo umeingia katika tendo la ndoa kwa kipindi cha kisichopungua miaka 3.




KUPUNGUZA HATARI ZA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI?

  • Pap tests.  Pata test hii mara kwa mara kuanzia mwaka 1 hadi 3,hii itategemea ushauri wa daktari wako,umri na majibu uliyoyapata ili kugundua chembe zisizo sahihi mapema na kuwahisha tiba.

  • Get an HPV vaccine (hii yashauriwa kati ya umri wa miaka 12 hadi 26.

  • Kuwa na mpenzi mmoja. Kitendo cha kuwa na mahusiano ya kimwili na mtu mmoja hupunguza hatari za maambukizi ya magojwa ya zinaa.

  • Tumia kinga (condoms). Hii husaidia kupunguza maambukizi ya magojwa ya  zinaa  


Shukrani/Thanks;

Ignatavicius, D.D. & Workman, M.L. (2010). Medical-Surgical Nursing: Patient-Centered Collaborative Care (6th ed.).
(WHO/ICO HPV Information Centre 2010)
https://www.imaworldhealth.org/archive/cervical
(WHO/ICO HPV Information Centre 2010)

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko