Skip to main content

MAJI NI UHAI !.

MAJI NI UHAI

Kama picha hii inavyoashiria, ardhi bila maji hunyauka na kupasuka,kadhalika mmea bila maji hunyauka na kufa. "Asilimia 60% hadi 75%  ya mwili wa binadamu imetawaliwa na maji" (Barry M. Popkin). Ijapokuwa kiwango cha maji hutofautina kutokana na umri au maumbile, mwili uliokosa  maji ni tishio kubwa kwa uhai.

FAIDA ZA MAJI MWILINI

  • Kurahisisha usagaji wa chakula
  • Kupunguza hatari za kupata mawe kwenye figo
  • Kupunguza maumivu ya arthritis hasa sehemu za viungo 
  • Kupunguza kuugua na maumivu ya mara kwa mara hasa kwa wagojwa wa circle cell
  • Kuondoa sumu mwilini au toxins
  • Kurutubisha ngozi ya mwili 
  • Kuwezesha kupata choo( normal bowel function)
  • Kupunguza mwili

DALILI ZA KUPUNGUKIWA MAJI MWILINI
  • Ukosefu wa mkojo au mkojo ulio wa rangi nzito ya njano
  • Maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) mara kwa mara
  • Kiu
  • Kupasuka kwa midomo au midomo huwa mikavu
  • Uchovu
  • Maumivu ya kichwa
  • Mapigo ya moyo yenye kishindo kikubwa na ya kasi
  • Kizunguzungu
  • Mzubao
  • kuchanganyikiwa, na hasa kwa wazee
  • Kupoteza fahamu

MAMBO YANAYOWEZA KUBABISHA KUPOTEZA MAJI MWILINI
  • Kuharisha
  • Kutapika
  • Homa kali
  • Pombe
  • Kutoka jasho
  • Kisukari
  • Kutokunywa maji ya kutosha
  • Baadhi ya dawa

KUNDI LINALOATHIRIKA ZAIDI
  • Watoto
  • Wazee
  • Wagojwa wa kisukari,alzheimer na mengineyo

NI WAKATI GANI KUWAHI KWA DAKTARI ?
  • Mtoto mchanga mwenye umri wa miezi 0 - 3
  • Kutapika au kuharisha uchafu wa rangi nyeusi au damu
  • Hali hii inapoambatana na homa
  • Mgojwa anapopoteza maji zaidi ya anayoweza kunywa.
  • Kutopata nafuu kwa mtu mzima kwa siku mbili hadi tatu na kwa mtoto asiye pata nafuu kwa muda wa  masaa 24

Shukrani
pictures
www.boloji.com http://
www.ncbi.nlm.nih.gov/
Ignatavicius, D.D. & Workman, M.L. (2010). Medical-Surgical Nursing: Patient-

Centered Collaborative Care (6th ed.).

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko