Skip to main content

MAKALA YA PILI YA TATIZO LA THYROID 'HYPERTHYRODISM'

Wapendwa wasomaji wangu, leo naomba turudi tena  darasani ili tuendelea na makala yetu iliyotangulia tukiongelea 'Tezi ya Thyroid' na matitizo yake.

Kwanza  tufahamu tofauti ya maneno yafuatayo;
  1. HYPO yamaanisha  Chini au Iliyochini (low)
  2. HYPER yamaanisha Juu  au Iliyojuu (high)

'HYPERTHYROIDISM' ugojwa ambao mara nyingi hutokea kwa wanawake  kati ya umri wa miaka “20 hadi 40” (Davies & Larsen, 2008).Japo ugojwa huu waweza tokea kwa wanaume,watoto na wanawake wa umri wowote, Hyperthyroidism hutokea pale tezi ya thyroid inapozalisha homoni za  thyroid kwa kiwango cha juu kupitiliza kipimo sahihi mwilini (thyrotoxicosis)

Kama tulivyoona kazi ya homoni za thyroid mwilini, zikihusika na  usimamiaji na utendaji wa metaboli wa mifumo  mbali mbali kama;  usagaji wa chakula,mapigo ya moyo, utumiaji wa calori na mingineyo, mgojwa wa hyperthyrodism anapozalisha homoni nyingi kupitiliza kipimo,hali hiyo humpelekea dalili zifuatazo ;

Upande wa Ngozi
  • Kutokwa kwa jasho kupita kiasi
  • Nywele nan vinyweleo huwa nyepesi vilaini
  • Ngozi ya mwili huwa laini,ya joto na yenye unyevu

Upande wa Mapafu
  • Kuhishiwa kwa pumzi bila shunguli yeyote ( Shortness of breath)
  • Pumzi nzito na ya haraka haraka
  • Kupungukiwa kwa uwezo wa kuipumua hewa baada ya kuivuta ( decrease vital capacity)

Upande wa Moyo
  • Mapigo ya moyo yenye kiherehere ( Kamusi  translation of Palpitation…...)
  • Mapigo ya moyo ya kasi
  • Mapigo ya moyo yaliyotoka nje ya mpangilio na yenye hitilafu
  • Maumivu ya kifua
  • Ongezeko la shinikizo la damu hasa namba ya juu (systolic pressure >120 mmHg )

Upande wa Tumbo
  • Ongezeko la njaa na hamu ya kula
  • Ongezeko la haja kubwa
  • Kupungua kwa mwili
  • Kupungua kwa protein kwenye damu
  • Ongezeko la sukari kwenye mzunguko wa damu

Upande wa Misuli ya Kiunzi cha Mifupa ( Musculoskeletal )
  • Udhaifu wa misuli
  • Kupotea kwa umahiri wa misuli

Upande wa Mishipa ya fahamu
  • Kuona maruerue au maono mara mbili( double vision,blurred vision)
  • Ochovu wa macho na uguu wa kustahimili mwanga mkali
  • Kupatwa kwa kidonda ndani ya  jicho  au maambukizi
          
  • Ongezeko la machozi,wekundu wa jicho
  • Kuzama  kwa sehemu ya juu ya jicho na kuzorota (eyelid)
  • Kutetemeka kwa mwili (tremors)
  • Ukosefu wa usingizi
  • Exophalomous
Exophalomous au Kutokwa kwa macho kwa tatizo lililozidai
                       











Upande wa Metaboli
  • Ongezeko la kasi ya metaboli
  • ugumu wa kustahimili mazingira ya joto
  • Homa ya chini au homa ndogo kati ya 99 -101 F
  • Uchovu

Upande wa Kisaikolojia
  • Upungufu wa umakini
  • Ukosefu wa utulivu au kuwa na mahangaiko
  • Hisia zilizo ngumu kuzizatiti au za kupita kiwaida

Upande wa Mfumo wa Uzazi
  • Kutoweka kwa siku za mwezi  au kupungua
  • Ongezeko la msukumo wa tendo la ndo


Dalili Nyinginezo
  • Goiter (kuvimba kwa tezi ya thyroid) japo yaweza kutokea hata kwa asiyekuwa na hyperthyroidism, mfano ukosefu wa madini Iodine,ujaa uzito,ugojwa wa Hashimitosh, na mengineyo mengi


Hyperthyroidism na Hypothyroidism ni ugojwa ambao unasimamiwa na mtaalamu ajulikanaye kama “Endocrinologist” ikimaanisha mtaalamu wa  tezi zinazozalisha homoni ndani ya mwili na kutumika katika mzunguko wa damu.


DALILI  NA MAFUNZO YA TOVUTI HII NI JITIHADA ZA KUELIMISHANA NA KUJIFAHAMU ZAIDI, USHAURI WA DAKTARI NA VIPIMO VYAKE NDIO UHAKIKA SAHIHI WA UGOJWA ULIO MWILINI.




Ignatavicius, D.D. & Workman, M.L. (2010). Medical-Surgical Nursing: Patient-Centered Collaborative Care (6th ed.).
 IMAGES;
www.medrevise.co.uk,blog.destroydiseases.com, blog.grannytherapy.comdxline.infonisarvtr.blogspot.com ,www.studyblue.com  ,
www.log-channel.net

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko