Skip to main content

UZIMA ULIAZIMWA, TUNZA KWANI NI AZINA






Shinikizo la damu hutambulika kama 'Silent Killer' kutokana na ukosefu wa dalili japo maafa yaendelea taratibu.Wengi wenye tatizo hili huwa nalo hata miaka bila dalili na hivyo kutishia usalama wa maisha . Shinikizo la damu hutuweka katika hatari za stroke, heart attack,upofu wa macho pamoja na kudhofisha utendaji wa figo au kuuwa figo ambayo kazi yake kubwa ni kuchuja uchafu mwilini.







CHATI HII YAASHIRIA VIPIMO VYA SHINIKIZO LA DAMU

    


Ili kugundua tatizo hili ni budi kupima. Ugunduzi na ufumbuzi wa mapema ni wa muhimu na hupunguza madhara yatokanayo na shinikizo la damu.

Baadhi ya dalili chache pale tatizo hili linapozidia ni;
  • maumivu ya kichwa, 
  • kizunguzungu,
  • kichefuchefu,
  • uhafifu wa kuona,
  • kupoteza uwezo wa kutambua
  • kuzimia. 
Pressure ya damu uhashiria kishindo cha damu katika ukuta wa mishipa ya damu mwilini. Kishindo hiki kinapokuwa kikubwa au juu kwa muda mrefu, kinasababisha mishipa ya damu kuwa hafifu. Uhafifu huu wa mishipa na vijishipa vidogo hasa katika ubongo hutishia maisha kwani huweza kupasuka na kusababisha kuvuja kwa damu na kusababisha stroke (Hemorrhagic stoke).


VIJISHIPA VIDOGO KATIKA UBONGO VILIVYOPASUKA NA KUVUJA DAMU KUTOKANANA TATIZO LA SHINIKIZO LA DAMU LISILO NA UANGALIZI.

                                        hemorrhagic stroke


Mishipa ya damu huweza athirika pia kutokana na ongezeko la cholesterol mbaya mwilini(Low density lipoprotein au LDL) na kusababisha mkusanyiko wa mafuta, chembe za damu na uchafu (Plaque) katika ukuta wa mishipa ya damu.Uchafu huu hugandamana na ukuta wa mishipa ya damu na hufanya ukuta huo kuwa mnene na mgumu (Atherosclerosis) .Hii yasababisha njia ya damu kuwa nyembamba na vigumu kwa damu kupenya. Njia hafifu huchangia damu kupenya kwa shida na kuhitaji msukumo mkubwa zaidi na hivyo kuulazimu moyo kuongeza nguvu na kasi. Ongezeko hilo huongeza kishindo cha damu katika mishipa kitu ambacho chawezapasua vijishipa vidogo,kuvujisha damu na kupata majeraha. Kama ilivyokawaida ya mwili kurepea majereha yake,mkusanyiko wa chembe za damu na madini hujikusanya katiaka eneo lililoathirika na kusababisha makovu ambayo hupunguza umahiri wa mishipa(flexibility) na kuifanya migumu. Mkusanyiko huo hutoa mvuto zaidi kwa cholesterol mbaya (LDL) kugandamana pamoja na mabaki ya calcium katika majeraha yaliyoyaacha makovu na hivyo kwa pamoja kugumisha na kuongeza unene wa ukuta wa mishipa.Mishipa ambayo ni migumu daima hufanya pressure ya damu kuwa juu kwani haina umahiri wa kutanuka na kujirudi pale msukumo wa damu unapoongezeka na kupungua kama inavyotakiwa.



Picha hizi zaashiria mishipa iliyogandamana kwa mkusanyiko (plaque) cholesterol mbaya na uchafu wa chembe nyingine mwilini,migumu na yenye nafasi ndogo kwa damu kupenya. (Atheroslcerosis).





Tatizo la uchafu(plaque) unaogandamana na ukuta wa mishipa ya damu ni uwezo wake wa kumegeka wakati wowote na kusafiri katika mishipa ya damu.Uchafu huu huwa ni kizuizi kwani waweza kukwama kwenye njia inayosafirisha damu katika sehemu mbali mbali za mwili.Hatari zaidi ni pale uchafu huu unapokwama kwenye mshipa unaoshuhulika na usafirishaji wa damu kwenye ubongo. Hapo ndipo mgao wa damu inayokwenda kwenye ubongo wapungua au kukatika na kusababisha ukosefu wa damu,oxygen na virutubisho katika ubongo na kutuweka katikahatari za stroke(Ischemic Stroke ).

Maafa ya mishipa iliyo na uchafu sehemu za moyo hutoa maumivu makali sehemu ya moyo pale mgao wa damu unapokuwa hafifu (Angina) na Heart Attack pale mgao wa damu unapokosekana kabisa.Kwani mishaipa ya moyo huitaji damu yenye kugawa oxygen na virutubisho muda wote ili kuweza fanya kazi yake vizuri.

Kwa upande wa mishipa inayosafirisha damu sehemu za miguu, ikiwa na kizuizi au (plaque)maumivu huwa makali baada ya kutembea kwa mda mfupi kwani mishipa inashidwa kupitisha damu ya kutosha yenye oxygen inayotosha kwa matumizi yaliyoongezeka wakati wa zoezi. Na mara nyingi mgojwa hujihisi nafuu pale anapopumzika au kuacha matembezi.Pia hushauriwa kuninginiza miguu pembeni ya kitanda(dangle the feet) ili kuruhusu urahisi wa msukumo wa damu yenye oxygen. (Peripheral Artery Disease)
 


SHINIKIZO LA DAMU LAWEZA SABABISHWA NA YAFUTAYO;
  • Umri
  • Ongezeko la cholesterol mbaya mwilini
  • Diet ya vyakula vya mafuta,nyama nyekundu,chumvi au vyakula hafifu (processed foods na  sukari nyingi)
  • Hasili ya rangi takwimu zaonyesha weusi ni wengi kuliko wazungu
  • Historia ya shinikizo la damu kifamilia
  • Aina tofauti za dawa
  • Kisukari
  • Gout 
  • Magojwa ya figo
  • Uvutaji wa sigara au tobacco.
  • Ulaji wa vyakula vyenye chumvi nyingi au Potassium kidogo.
  • Ukosefu wa mazoezi ya mwili .
  • Unene wa mwili.
  • Utumiaji wa pombe kupita kiasi (>2/siku kwa mme au  >1/siku kwa mke)


KINGA AU TIBA

Wengi tunakubali kwamba kinga ni bora kuliko tiba kwani mti haunyauki siku moja, huwanza na tawi hatimaye mti huporomoka. Mbali na dawa za  shinikizo la damu, hatuna budi kubadili  mfumo  wa maisha kama;
  • kupunguza chumvi, mafuta,sukari au processed foods.
  • Acha uvutaji wa sigara,
  • Punguza pombe 
  • Punguza uzito wa mwili.
  • Fanya  mazoezi ya mwili walau mara 4 hadi 5 kwa wiki
  • Ongeza mboga,matunda  na vyakula asilia (ambavyo havijakobolewa na sio vya makopo)
  • Pika mara kwa mara kuliko kula migahawani
  • Punguza nyama choma,nyekundu na za mafuta 

 



Wataalamu wanashauri kupima pressure mara kwa mara ili kugundua mapema pale unapokuwa na mabadiliko na kufanyia marekebisho.



Shukrani;
www.naturalhealthadvisory.com 
http://www.cdc.gov/bloodpressure/
http://www.cdc.gov/stroke/types_of_stroke.htm
http://www.nhlbi.nih.gov/health/health-topics/topics/atherosclerosis
http://watchlearnlive.heart.org/CVML_Player.php?moduleSelect=hemstrh




   

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko