Skip to main content

KIZAZI CHA DIASPORA KUWANIA NAFASI KATIKA CONGRESS

Will Jawando

Will Jawando,mkewe Michell Jawando na watoto wao Alia,Addison and Ava

Will Jawando ni mzaliwa wa Silver Spring,Maryland kwa familia ya Mwanadiaspora 'Jawando' kutoka Nigeria na Mama ambaye ni mwenyeji wa Marekani. 
Will amepitia changamoto mbalimbali zilizo katika jamii na hata kumpoteza rakifi yake wa pekee katika shambulizi la risasi. Jambo hili lilimpelekea kukabidhi maisha yake katika utoaji huduma na utatuzi wa matatizo ya jamii na kuweka jitihada katika elimu .

Will Jawando alihitimu elimu ya juu na shahada ya Sheria, ambapo aliendelea na utoaji huduma kwa jamii katika ngazi tofauti hususani; Legislative Staffs House of Democratic chini ya uongozi wa Nancy Pelosi,US- Senator Barack Obama na ngazi nyingine mbalimbali.

Kama Mwanadiaspora ninayetambua changamoto za huduma ya afya kwa wasio na vibali vya kuishi nchini ,Will Jawando alinigusa zaidi pale aliponieleza kuhusu baadhi ya changamoto za wahamiaji akisema kuwa, mbali na ukosefu wa hati halali , wahamiaji wote hushiriki katika ulipaji wa kodi na hivyo kuchangia maendeleo ya Taifa. Swala hili na mengine mengi ni miongoni mwa maswala ambayo ana nia ya kuyapa kipaumbele.

Will Jadando kupitia Democratic party anasimama katika nafasi ya Congress, kama mtoto wa Mwana-Diaspora kutoka Afrika na wa pili tokea Mhe. rais Barak Obama.  
 
Mhe rais Barak Obama akisalimiana na familia ya Jawando na kumkaribisha mtoto wao mpya.

Kwa habari zaidi tembelea
http://willjawando.com/
Images
willjawando.com
Story;NesiWangu

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko