Katika sehemu hii ya pili, Harriet Shangarai wa NesiWangu Media anazungumza na mwanaharakati mwenye Albinism Babu Sikare kuhusu maisha yake na shirika lake la 'Afrobino' la kupambana na changamoto inazowaguwasa walemavu wa ngozi katika nchi zinazoendelea.
0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha matumizi ya baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari chini ya 70 mg/dL au 3.9 mmol/L chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili...
NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja kati ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi uanzishaji wa mwendo ( conduction of electricity) katika misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwang...
Je unahisi dalili zifuatazo? Kukoroma kwa sauti kubwa hata kusumbua mwenzio Uchovu unapoamka japo umelala usiku kucha Maumivu ya kichwa unapoamka Mdomo au koo kuwa kavu unapoamka Kusimamisha pumzi usingizini Kuzinduka mara kwa mara usingizini ukitafuta pumzi, kukabwa au kukohoa.? Usingizi wa mara kwa mara unaoingiliana na kazi,masomo,usalama barabarini. Ugumu wa kukaa macho kwa mda wakati wa vikao, kujisomea au kutazama TV Dalili kubwa ya Sleep Apnea ni kukoroma kwa sauti ya kuzidia na hata kukera mwezio Pict.Courtesy of http://always-healthy.com/sleep-apnea Harvard School of Medicine yatoa ufafanuzi zaidi kuhusu ‘Kukabwa na Jinamizi’ a.k.a 'Obstructive Sleep Apnea' (Ukosefu wa pumzi Usingizini) Video courtesy of Harvard School of Medicine UFAFANUZI NA ATHARI ZA UKOSEFU WA PUMZI USINGIZINI Binadamu yeyote anaposinzia mwili hulegea na viungo hupumzika.Ulegevu...
Comments
Post a Comment