Skip to main content

DAWA BANDIA ZINAANGAMIZA, WANANCHI WAFUNZWE KUZITAMBUA


8th November 2014
Print
Biashara ya dawa feki au bandia ni  moja ya uwekezaji haramu lakini unawapa wahusika utajiri mwingi licha ya kwamba inaweza kuwa chanzo kikubwa cha  maangamizi na mauaji duniani.

Athari za biashara hii  ni nyingi lakini inasababisha usugu kwa maradhi na vifo na kuhujumu afya ya mtumiaji kwa kuwa anatumia fedha lakini haponi na matokeo yake ni kifo.

MADHARA
Matokeo mabaya katika eneo hili ni kutumia dawa lakini isiyokupa tiba hali inayojulikana  kitaalamu  kama Therapeutic failure.

Hali hii inatokea kwa sababu dawa zinashindwa kutimiza lengo la tiba kutokana na ama kuwa na kiasi kidogo cha dozi kilichomo ndani yake au hakuna dawa inayokusudiwa kuua vimelea vya maradhi yanayomsumbua mhusika licha ya kwamba anatumia dawa hizo.

Kwa ujumla dawa hizi bandia zikitumika zinashindwa kuleta tiba au kumponyesha mgonjwa kunasababisha pengine aache au kusimamisha matumizi ya dawa hiyo na kwenda kwenye dozi nyinginge na kwa ujumla kama mfuatano huo utakuwa ni wa kumeza dawa bandia ni wazi maisha ya mgonjwa yanatishiwa kwa vile hatapona.

Fikiria msomaji kuwa na taifa la watu wagonjwa wasiopona maradhi kila mmoja ana kifua kikuu (TB) isiyopona mwenye vichomi au nyumonia kadhalika haponi wakati  homa ya tumbo, malaria na magonjwa ya njia ya mkojo (UTI)  pamoja na maambukizi ya via vya uzazi (PID) nayo yanakuwa sugu na watu wanazidi kuumwa licha ya kutibiwa kwa gharama kubwa  na wataalamu. 

MADHARA KIKEMIKALI
Kuwapo kwa dawa bandia kunadhuru figo kwani inawezekana madawa hayo yanatengenezwa na kila kemikali bila kuzingatia viwango yanaishia kwenye figo za binadamu.

Sumu hizo zinasababisha madhara kwa watumiaji kwa mfano dawa za vikohozi zilidhuru watu wengi nchini Haiti, Bangladesh, Nigeria, India na  Argentina .

Ni mifano kwa watu waliodhurika na kutumia dawa bandia ambazo licha ya kuwa  feki zilikuwa na sumu na kuharibu figo zao. Lakini pia mwaka  2008 wagonjwa zaidi ya 62 walikufa nchini Marekani kutokana na kutumia dawa ya kusafisha figo iliyokuwa imetengenezwa China.

HUJUMA UCHUMI
Dawa feki  au bandia ni hujuma kwa uchumi kwa vile idara za afya zinatumia fedha nyingi kuagiza dawa ambazo hazina tiba matokeo yake ni fedha kupotea , magonjwa kuchachamaa, nguvu kazi kudhoofika  bila kusahau usugu wa vimelea.

KUSAMBAA DAWA BANDIA
Chanzo kikuu cha kusambaa dawa hizo ni rushwa. Kampuni za dawa na  mamlaka za kiserikali zinazohusika na usimamizi wa uzalishaji,  uuzaji na  uagizaji wa dawa kuongozwa na watu wasio waadilifu ni chanzo cha tatizo hilo la kuenea rushwa kwenye sekta ya dawa. Ukosefu au kutegemea  teknolojia  duni kutambua maradhi vikiwamo vifaa vya maabara na wataalamu wanaojua kuchunguza na kutambua dawa feki ni eneo linakuza biashara  haramu ya dawa feki.

Kukosekana utashi wa kisiasa kudhibiti biashara hiyo nako kunachangia. Hii ni dhahiri kwa sababu licha ya kuwa ni uhalifu wa kutisha na wenye madhara sawa na maangamizi haupigiwi kelele wala kuzungumziwa kama ulivyo uhalifu mwingine mfano matumizi ya dawa za kulevya na ugaidi.

Dawa bandia zinawekewa lebo feki kwa mfano  unga wa mahindi unaweza kutengenezwa kama  vidonge vya dawa inayotibu maradhi ya amiba na kwa makusudi ikabandikwa lebo na kuuzwa kama dawa wakati siyo,Dawa bandia ni biashara hatari ya sirini itafahamika na uchunguzi kuanzisha endapo  vifo vitatokea kama hakuna janga  inaendelea.

WAATHARIWA
Nchi changa ndizo zinazoumizwa zaidi kwa vile takwimu  za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa karibu asilimia 50 ya dawa kwenye mataifa hayo ni bandia na katika nchi zilizoendelea  ni kiwango kidogo cha asilimia moja,.

“Afrika na nchi za Asia zimeathirika zaidi na dawa hizo ripoti ya WHO mwaka 2005 ilikadiria kuwa kati ya asilimia 10 na 25 ya dawa zinazozunguka kwenye nchi hizo ni bandia”

Bara linaloumia zaidi ni  Afrika  likifuatiwa na Asia  na Amerika ya Kusini

AINA ZA DAWA BANDIA
WHO inasema karibu kila dawa imetengenezewa dawa bandia kuanzia antibiotics (viuasumu), dawa za saratani,  na zile za kutibu viungo vya ndani. Kwa nchi maskini athari ni mbaya zaidi kwa kuwa dawa  bandia zinazosambazwa ni pamoja na antibiotics ambazo hutibu maradhi makubwa yanayoshambulia.

Kwa mataifa yaliyoendelea dawa feki zinazopatikana ni pamoja na za saratani, za kupunguza mafuta mwilini, dawa za mzio (aleji) za masuala yanayohusiana na vichochezi (homoni) pamoja na zile za kuongeza nguvu za kufanya ngono kwa  upande wa wanaume.

Tiba feki za  malaria zimesambaa mno eneo la Afrika na Asia zikiwamo hata zile za kufubaza makali  ya Virusi Vya Ukimwi za VVU za ARVs.

Kwa hiyo wananchi wanapoona kuna kitu hawakielewi kuhusu au wanapozitumia dawa hawaponi, au zinanuka, pengine zinamomonyoka au zina kasoro kama kubadilika rangi, kutoa maji na kulowana  waeleze taarifa kwenye mamlaka za kudhibiti ubora wa dawa.

Makala hii imetafsiriwa kutoka kwenye jarida la Research Journal of Medical Sciences.
SOURCE: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko