Skip to main content

EBOLA ni nini?

 »  » EBOLA ni nini?
Leo ni Jumatatu, tarehe 14 Shawwal Mwaka 1435 HIJIRIA

Sawa na 11/8/2014



EBOLA ni nini?

Category: Makala | Date: 6-06-2014, 04:38 | Views: 190
Ebola ni ugonjwa unaosababishwa na homa ya ubongo, na ni moja ya magonjwa yanayotishia uhai wa binadamu.Ugonjwa huu ulijulikana kwa mara ya kwanza, barani Africa mnamo miaka ya 1970 na mpaka sasa ugonjwa huu umeua zaidi ya watu 1,500.
Historia inaonesha Ebola imeua watu kwa asilimia 90, madaktari wameripoti kua ugonjwa huu umekua “tishio kwa binadamu”.

Dalili 
Wengi wao wanaopatwa na virusi hivi vya ebola hupata: 
1. Dalili kama za mafua
2. Homa
3. Uchovu wa ndani ya mwili
4. Misuli kuuma
5. Kichwa kuuma
6. Koo kuvimba.

Baadae muathirika huanza:
1. Kutapika
2. Kuharisha
3. Kupata upele 
4. Ini na figo kutofanya kazi vizuri
5. Kuvuja damu ndani ya mwili
6. Kutokwa na damu kwenye tundu za mwili Mfano; macho,puani nk.
EBOLA ni nini?

mmoja wa muathirika wa ebola akionesha jinsi mkono wake ulivyo jaa epele wa maji

EBOLA ni nini?

mmoja wa muathirika wa ebola akiwa kwenye hali ya kutokwa na damu katika sehemu za puani


MUHIMU KUTAMBUA
Ugojnwa huu hauna tiba, yani kwa maana toka ugundulike miaka ya 1970 haujapata tiba mpaka hivi sasa.

USAMBAAJI WAKE
Ugonjwa huu upo kwa pande zote mbili kwa maana ya binadamu na wanyama na husambaa kwa njia kugusa damu ilioathirika, au majimaji, kidonda kilochoathilika.

Aidha, katika mazishi mengi ya kiAfrica wafiwa hua na tamaduni ya kuaga mwili wa marehemu kwa kuugusa, hii ni njia kubwa sana ya kusambaa kwa ugonjwa huu, kwani huu ugojwa unaishi hata kwenye mizoga ya wanyama na maiti za binadamu. Tafiti zinasema kuna aina ya popo wapo Africa wanabeba virusi hivi, popo hawa hula matunda mbalimbali, na pia huliwa na wanyama mbali mbali, kwa njia hii maambukizi ya ugonjwa huu unaweza kua mkubwa zaidi.

Mnamo mwaka 1976 Ebola iligundulika ghafla mara mbili katika nchi ya Sudan na Demokrasia ya Congo (DRC). Mlipuko huo wa ebola nchini DRC ulikua katika mto Ebola, ambapo ugonjwa huo ulipata jina hapo.
Mpaka sasa zaidi ya watu 1500 kutoka maeneo mbali mbali mwa bara la Africa washapoteza maisha kutokana na ugojwa huu.
Mungu atulinde Tanzania na ugonjwa huu, Mungu atuepushie Africa na Janga hili.

SHUKRANI
 » 

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko