Skip to main content

AJICHUBUAE HUKUSUDIA KUTATUA TATIZO LA MTAZAMO NA SIO TATIZO LA RANGI YA NGOZI !!.







Binadamu ni kiumbe anayependa kukubalika. Pengine, hata zaidi ya anavyojikubali mwenyewe.Iwapo mwanadamu anahisi kutokukubalika katika jamii inayomzunguka, huwa mpweke,mnyonge na  mwenye msongo wa mawazo.
Hisia ya kutaka kukubalika humfanya binadamu afanye lolote hata ikibidi kubadilisha muonekano wake ilimradi akubalike katika jamii inayomzunguka.Hali hii inaonyesha wazi kwamba mazingira yetu yana nguvu kubwa katika kuchangia fikra, matendo na imani zinazobobea katika  tamaduni zetu.


Faida za hisia hizi ni kwamba, zikiambatana na utashi mzuri, ufahamu binafsi na upeo, huleta mafanikio makubwa kwa mtu na kwa jamii .Hasara za hisia hizi ni pale zinapoambatana na ukosefu wa ufahamu binafsi, mwongozo potofu na  upeo duni,  kwani huwa ni chanzo cha  majanga yanayotuongezea uduni wa maisha.


Baadhi ya mitazamo duni inayotuathiri ilisababishwa na ukoloni uliotufunza chuki binafsi na kutuacha na pigo kubwa la fikra. Pigo hili limetuletea imani potofu na madhari mengi katika jamii zetu .


KABLA BAADA









  BAADHI YA TEKINOLOJIA,DAWA NA VIPODOZI VYA KUBADILI RANGI














TANNING BOOTH AU JOKOFU LA KUBADILISHA RANGI YA NGOZI







SINDANO NA VIDONGE VYA GLUTATHIONE VYA KUBADILI RANGI YA NGOZI

VIKIFWATIWA NA BAADHI YA ATHARI NA MADHARA YAKE MWILINI

iv-glutathione-side-effects-belo-medical



Stevens-Johnsons Syndrome

Hali hii hutokana na Jibu la Mwili kwa Dawa au Maambukizi


Toxic Epidermal Necrolysis


BAADHI YA VIPODOZI VITUMIKAVYO NA VYENYE MCHANGANYIKO WA MADAWA MAKALI
  • Hydroquinone’  
Dawa hii huuwa chembe zinazohusika na uzalishaji wa rangi ya mwili Melanin na   kuondoa   ganda la nje lenye kutukinga na mionzi mikali ya jua na hivyo kuruhusu ganda la ndani ‘‘Dermis layer’  kupokea mionzi mikali ya jua  na kutupelekea hatari za  kupata saratani ya ngozi. 
Madhara ya Matumizi Hydroquinone kwa Mda Mrefu; 
  • Madoa sugu ya bluu au meusi mwilini
  • Upungufu wa ulaini na umahiri wa ngozi ( loss of natutre skin elasticity)  
  • Ugumu wa majeraha kuponya
  • Pamoja na kupata mkojo na jasho lenye harufu  ya samaki.

Baadhi ya majina tofauti yatumikayo kwenye vipodozi vyenye hydorqunine ni 1,4 Benzenediol,QuinolBenzene-1,4-Diol,p-Diphenol,p-Dihydroxyl,benzene,Hydrochinonep,Hydroxylhenol,Hydrochinonium,Hydroquinol,Tequinol,Monobenzyl eth.





Makala Itakayofuata tutaangali madawa mengine kama Mercury,Steroids na madhara yake mwilini.

SHUKRANI







http://www.kanyetothe.com/

  
http://www.kanyetothe.com/





































Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko