Skip to main content

LEO TUNAZUNGUMZIA HALI IJULIKANAYO KAMA MSONGO NA MFADHAIKO WA KIAKILI ( STRESS)

  
            


                        Maisha ya leo sio ya jembe na panga lakini  jasho lake ni kali.Wengi tuna kazi  nyingi na muda ni kidogo.Japo stress kidogo yaweza kuimarisha utendaji wetu,stress ikizidia au ya muda mrefu huwa ni hatari kwa usalama.


Msongo na mfadhaiko wa kiakili (Stress) tunaohisi, ni jibu au tokeo la mwili uliotahadhariwa kuwa hali inayoendelea imefika kiwango kinachozidi na kuelemea na hivyo mwili wapewa tahadhari kujiandaa kukabiliana na hali yeyote itakayojitokeza (defence mechanism). Hali hii hupelekea maumbile ya mwili kujiandaa kwa kuzalisha hormones ziitwazo; adrenaline, cortisol na norepinephrine ambazo  kwa haraka hupandisha shinikizo la damu ( blood pressure), mapigo ya moyo, pumzi na kuongeza sukari mwilini ili misuli ipate nguvu ya kukabiliana na shambulizi linalohisiwa. Iwe ni  kupigana,kukimbia au kupata butwaa (“fight , flight or freeze response.”)




Tatizo ni pale stress inapokuwa ni ya muda mrefu na kusababisha homoni tulizozitaja hapo juu kuwa katika kiwango cha juu kwa mda mrefu mwilini. hali ambayo hufanya mwili usimamishe baadhi ya shughuli nyingine za kawaida kama usagaji wa chakula,kinga ya mwili, na kuelekeza nguvu katika pambano linalohisiwa kwa kuzidisha hormone za stress mwilini  ambazo ni chanzo cha magojwa yafuatayo;
  • high blood pressure
  • magonjwa ya moyo
  • Kisukari
  • Kupunguza umahiri wa kinga ya mwili(immune system)
  • Kupunguza uchujaji wa maji mwilini kama ADH hormone
  • Msongo wa mawazo( depression)
  • Eczema au vipele vya kuwasha vay ngozi
  • Matatizo ya kulala au usingizi
  • Maumivu kwa ujumla
  • Kuongezeka kwa uzito wa mwili au unene


NI VIPI KUKABILIANA NA STRESS ?


  • Weka ratiba ya mazoezi ya mwili ya mara kwa mara(Kwani mazoezi husaidia uzalishaji wa hormone za kujihisi vizuri na hata kuondoa maumivu kama (Endorphins,Dopamine,serotonin)
  • Chukua mda utoke kwenye desk na kutembea
  • Chagua fikira safi na zenye kukupa nguvu ( think positive)
  • Weka mziki mwororo kama office yaruhusu
  • Jifunze kutokuza mambo wala kuchukulia vitu  kibinafsi (personal)
  • Tumia chai au kahawa
  • Kuwa na marafiki au watu mtakaotegemeana na kusaidiana na kushauriana
  • Epuka mazingira ya kukuleta stress
  • Pata usingizi wa kutosha
  • Weka ratiba na kuifata ili kuepuka kazi za kukurupuka ( do not procrastinate)




NINI DALILI ZA STRESS

  • Hasira za haraka
  • Wasiwasi
  • Kutoweza kuwa makini( poor concentration)
  • Ugumu wa kutulia ( inability to relax)
  • Huzuni
  • Kulia bila sababu au kwa urahisi



Nukuu
Centers for Disease Control and Prevention CDC
Picha:
www.blackhairinformation.com
www.huffingtonpost.com
Thinkstock / Maridav
OWN

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko