Skip to main content

Mtambuwe mwakilishi wa wilaya yako Mhe. Jheanelle Wilkins!.



District 20 ni Wilaya inayojumuisha Silver Spring, White Oak na Takoma Park. Wilaya hii hujulikana kwa idadi kubwa ya wahamiaji hasa wale wa jamii ya ki-Afrika. Mchakato wa uchaguzi uliendelea kwa siku tatu mfululizo, ambapo wagombea walipata fursa ya kujieleza,kujibu maswali kutoka kwa jamii na kamati maalumu ambayo ndio yenye usemi wa mwisho na mamlaka katika mchakato huo.

Kamati hiyo hujulikana kama Montgomery County Democratic Central Committee (MCCDC) yenye wajumbe 28 akiwemo Mhe. Jheanelle Wilkins ambaye ndio  mshindi wa mchakato huo.
Mhe. Jheanelle Wilkins ni mzaliwa wa Jamaica na muhamiaji aliye na malengo ya kupambana na sheria kali zinazopanga kutenganisha familia za wahamiaji katika utawala mpya ulioko chini ya rais mteuliwa ajulikanaye kama  Donald Trump.

Baadhi ya waliogombea nafasi hiyo kutoka barani Africa ni pamoja na Daniel Koroma ambaye ni mzaliwa wa Sierra Leone na mtumishi wa umma katika kata ya Montgomery. Daniel Koroma ambaye alitolewa katika round ya pili amekuwa mfano kwa jamii ya waafrika na ishara kubwa kwa wenyeji kwamba jamii ya wa-Afika ipo hai na ina uwezo mkubwa na mwamko  wa kushiriki katika meza inayotengeneza na kuamua sera zinazohusu  mipango yote endelevu inayotumia kodi zinazochangwa na kila mmoja aishieye hapa nchini.


                                                           Kwa Picha Zaidi




                                                                        Daniel Koroma


Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili...

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwang...

.KUKABWA NA JINAMIZI A.K.A "SLEEP APNEA"

Je unahisi dalili zifuatazo? Kukoroma  kwa sauti kubwa hata kusumbua  mwenzio Uchovu unapoamka japo umelala usiku kucha  Maumivu ya kichwa unapoamka Mdomo au koo kuwa kavu unapoamka  Kusimamisha pumzi usingizini Kuzinduka mara kwa mara usingizini ukitafuta pumzi, kukabwa au kukohoa.? Usingizi wa mara kwa mara unaoingiliana na kazi,masomo,usalama barabarini. Ugumu wa kukaa macho kwa mda wakati wa vikao, kujisomea au kutazama TV Dalili kubwa ya Sleep Apnea ni kukoroma kwa sauti ya kuzidia na hata kukera mwezio Pict.Courtesy  of http://always-healthy.com/sleep-apnea  Harvard School of Medicine  yatoa ufafanuzi zaidi kuhusu ‘Kukabwa na Jinamizi’ a.k.a 'Obstructive Sleep Apnea'  (Ukosefu wa pumzi Usingizini) Video courtesy of Harvard School of Medicine UFAFANUZI NA ATHARI ZA UKOSEFU WA PUMZI USINGIZINI Binadamu yeyote anaposinzia mwili hulegea na viungo hupumzika.Ulegevu...