Skip to main content

MOJA YA MAJIPU YANAYOIKUMBA JAMII YETU.


Kutoshiriki na kujitolea  katika kuchangia  rasilimali kwa ajili ya matumizi yetu sote kwa ujumla ni  jipu linaloikuimba jamii yetu. Pengine labda ni tamaduni  au  binafsi hayajatusibu. Lakini, pale yatakapotukuta  sio tu  familia, ndugu, jamaa au marafiki bali jamii kwa ujumla huangaika kutafuta namna ya kupata huduma au  kukidhi garama za  tiba ambazo hazishikiki.

Sio vibaya kwa jamii yako kuwa ya msaada, bali njia hiyo  haileti utatuzi endelevu. Tufahamu kwamba tuko katika  nchi iliyoendelea na yenye mifumo mbali mbali iliyodhihirika kutoa  utatuzi endelevu kwa  watu kama sisi na wengine wengi wasio na ndugu,rafiki au jamii inayowajali.

Hivyo basi pale tunapoombwa kushiriki katika jitihada za kukusanya senti za kutusaidia kwa ujumla au HARAMBEE basi tufanye kama tunavyochangia harusi zetu, tukijitokeza  kwa wingi,  tena kwa vifijo na ngoma, Susan G.Komen hutoa msaada mkubwa tu hata kwa ndugu zetu wahitaji nyumbani Tanzania na yeye hushiriki binafsi na kuona bendera zinazopeperushwa.

 IDADI YETU NI KUBWA KULIKO KUNDI AMBALO HUONEKANA MARA KWA MARA KTK PICHA
   HONGERA TEAM TANZANIA
  NI VYEMA KUSHIRIKI KATIKA PAMBANO DHIDI YA GOJWA LA SARATANI .

KUJIANDIKISHA tuma text ya jina na e-mail yako kwenda
 240 -615 - 6042
240- 672 - 1788
tunatanguliza shukurani
See you May 7th, 2016

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko