Skip to main content

JE WAFAHAMU NAMNA YA KUFANYA UCHUNGUZI BINAFSI WA MATITI

Breast Self-Exam (BSE) Uchunguzi Binafsi wa Matiti ni
Uchunguzi unaotuwezesha kutambuwa umbile la kawaida la titi na hivyo kutupelekea kutambua mabadiliko endapo yatatokea.Ushauri wa Jamii ya Utafiti wa saratani ya matiti nchini Marekani washauri wanawake kufanya uchunguzi binafsi wa matiti kuanzia umri wa miaka 20. Uchunguzi wa litaalamu wa Mammogram mara moja mwaka washauriwa kwa Wanawake kuanzia umri wa miaka 40. 
Si ajabu kwa matiti mawili kutofautiana kimaumbile, tofauti tunayozungumzia hapa ni ile yenye kuleta mabadiliko upande mmoja, bila mabadiliko hayo kuonekana upande wa pili. Yashauriwa kufanya Uchunguzi Binafsi wa Matiti kila mwezi kati ya siku 3 hadi 5 baada ya kumaliza siku mwezi.

RIPOTI DALILI ZIFUATAZO KWA DAKTARI
 
  • Titi lenye wekundu, mpauko au mchubuko
  • Uororo usiowiana
  • Ngozi iliyokunjamana
  • Ngozi yenye unyeleo (pores) kama ganda la chungwa
  • Kudidimia kwa chuchu
  • Maumivu
  • Vipele
  • Muwasho
  • Ongezeko la unene wa ngozi ya titi au kwapa
  • Uvimbe katika titi au chini ya kwapa
  • Mabadiliko katika chuchu yakiwemo mwelekeo; Kawaida chuchu ya kushoto huelekea kushoto na chuchu ya kulia huelekea kulia.


HATUA ZA  UCHUNGUZI BINAFSI WA  MATITI;

1.Simama wima mbele ya kioo na kisha tizama na  chunguza muonekano wa umbile la titi  na ripoti mabadiliko yafuatayo kwa daktari;


https://lh4.googleusercontent.com/2RsH6RtYd70ytDRKBQQI9Ii5Jw6kW0pBIidzBoQMqLlnoITQQu_2QgIco0EUo4nlv-GdbIhAM5ups-0FX4nGP7MGzltgy0z70cgBO9XHYiOFEIkHtZYgDqqkP8fR3b3HqgOwG_E
(2)Mikono kiunoni  (hakikisha mabega yamenyooka) rudia hatua za mwanzo na jeuka taratibu upande  hadi upande  ili kukagua sehemu za ukingoni mwa titi
https://lh4.googleusercontent.com/VFnW8LjMchfVlbf4-2TOY7HUklXfk35pl42SKNC735O4bUd7FMJ2zBM0KVJwbMW39EFlmYXzEzkRQV9DaTxHR0IeiQN99m5sioit_IvTNzBzcZo7xFwabkLXg8TTdudA-mu5EAg


( 3) Mikono juu ya kichwa endelea kuchunguza, kisha mkono Mmoja baada ya mwingine, Tumia viganja vya vidole vitatu vya kati, papasa kwa kishindo cha kadri  mzingo wote wa titi bila kusahau  eneo la kwapa na  kifua.
https://lh6.googleusercontent.com/kFQlYEP9vbeLMmXYJn1prdrETjmAC65z8yURULzEvso5k4DqUGSNs_OxkRo7d0Q-tTXZXA6IqVYcTreTyHC5QaqKwnTFfzqu-WDBE9ZSKx4xBwHzC4KW3wA7RJf5O93ivt3-ZRY




Tumia njia zifuatazo a)Mduara au Mzunguko b) Juu/Chini

http://my.clevelandclinic.org/ccf/media/Images/HIC/3990_6A.jpghttp://my.clevelandclinic.org/ccf/media/Images/HIC/3990_10.jpghttp://my.clevelandclinic.org/ccf/media/Images/HIC/3990_6B.jpg
4. Lala chali na weka mto chini ya bega. Kwa uchunguzi wa titi la kushoto, weka mto chini ya bega la kushoto na tumia mkono wa kulia. Vilevile kwa titi la kulia weka mto chini ya bega la kulia na tumia mkono wa kushoto) Hii husaidia tishu za titi kusambaa na kurahisisha uchuguzi.Fuata  maelezo yaliyotangulia katika kipengele cha tatu.
https://lh3.googleusercontent.com/ALn5fZGwau39pUDA6WsxHWoBE8E9aI9AcEwRQ7Wq2ItXVzVftQCwSiz7wpvvwDEJYHr1geZ8w8Ugav5sWjESmlQIwNPgqBI4y3VjPmTJ_MBrUSIZaKtPnsS0lC8J4EssigeUAnU http://my.clevelandclinic.org/ccf/media/Images/HIC/3990_9.jpg
5. Bonyeza chuchu ili kuona kama inatoa majimaji ya aina yeyote;yawezakuwa maji meupe, maziwa, usaa au damu (Kipengele hiki ni kwa wale wasio wajaa wazito au wanye nyonyesha).
http://my.clevelandclinic.org/ccf/media/Images/HIC/3990_5.jpg

          Saratani ya Matiti yaweza kutibika endapo imegundulika mapema.

Kwa wale wasio na bima ya afya na wanahitaji Mammogram au huduma ya juu ya utafiti wa saratani ya matiti, tuma text kupitia 240 672-1788 au tembelea African Women Cancer Awareness Association (AWCAA); www.awcaa.org


Images
Breast cancer.org
wcfcourier.com
Many More....Thanks for the effort 
Many more;

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko