Skip to main content

DRIVE-BY-SHOOTING!

Ni uhalifu  unaojumuisha gari lililo katika mwendo huku likimwaga risasi kwa raia. Uhalifu huu wa kinyama ni sugu katika baadhi ya maeneo, hasa kwa ndugu zetu wanaoshiriki katika Magenge ya vurugu au gangs. Mbaya zaidi, uhalifu huu hutokea ghafla na kuchukuwa maisha ya raia wasio na hatia.

Leo nilinusurika maisha nikiwa  katika eneo la 7th st. NW DC. Ilikuwa  mida ya saa kumi jioni ambapo shambulizi la ghafla la risasi zilizolia kama kifaru zilimiminika kutoka kwa gari isiyojulikana. Raia  walikimbia , wengine kujificha na hata kulala chini ili kuokoa maisha .

Baada ya dakika chache, kikosi kikubwa cha Police na Emergency Response 911, kiwasili  na kutoa huduma ya haraka kwa majeruhi. Taarifa ya baadaye  ya Fox 5 News, iliripoti kuwa kijana wa umri wa miaka 23,Mathew Shlonsky ambaye alikuwa mpita njia  alifariki dunia baada ya kufikishwa hospitalini.

 photo
                  Polisi wakiongea na raia ili kupata machache yatakayoweza saidia uchunguzi wao.
     
                                                Mtaa huu ulifungwa kwa mda wa masaa

                                         Baadhi ya Ambulance zilizofika katika eneo hilo

Magari yaliyokuwa katika eneo hilo yalijumuishwa katika tukio  la uhalifu na hivyo haikuruhusiwa kwa  mtu yeyote kufika kwenye gari yake au  kuichukuwa  hadi uchunguzi utakapomalizika. Japo malalamiko yalitoka kwa walionyimwa ruska ya kuchukuwa gari zao, wengi tulishukuru Mungu kwa kunusurika katika uhalifu huo wa kutisha.


Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko