Skip to main content

MSIMU WA MAFUA MAKALI MAREKANI


Habari kutoka  kituo cha kudhibiti magojwa nchini Marekani  “Center for Disease Control” ( CDC) 2014 -2015, inatufahamisha kuhusu kipindi cha mafua makali ( Severe FLU Season).
Kipindi hiki kilichotawaliwa  zaidi na virusi vya A H3N2,hujulikana  kwa kuleta homa kali, ongezeko la  wagojwa mahospitalini na hata vifo. CDC inatukumbushia umuhimu wa kila mmoja kupata Chanjo  ya Flu na  tiba ya haraka ya kupamba na  virusi (Anti-viral drugs  treatment)  hasa kwa watu walio na kinga hafifu.  Anti-viral drugs husemekana kuwa mahiri zaidi kati ya masaa 48 baada ya dalili za flu kujitokeza mwilini .
Mabadiliko ya virusi kimaumbile (genetic) huchangia kupunguza umahiri wa chanjo japo wengi  waliofanikiwa kupata chanjo huwa na maambukizi  afueni.   CDC imeongeza kusema, FLU ya kipindi hiki iliyotawaliwa na  Influenza A H3N2 ilitokea  miaka ya 2012-1213, 2007-2008 na 2003-2004  vipindi ambavyo viliongoza  kwa idadi ya vifo katika ya miaka 10 iliyopita.
NINI DALILI  ZA FLU
  • Kukohoa au kukwaruza kwa koo
  • Maumivu ya kichwa
  • Baridi
  • Kuumwa mwili au uchovu wa mwili
  • homa
  • Mafua ya maji au yenye  kubana
NANI YUU HATARINI
  • Watoto chini ya umri wa miaka 5, wazee kuanzia miaka 65
  • Asthma
  • Wejawazito
  • Wagojwa ya Kisukari,  Figo,Ini,Circle cell
  • Magojwa yenye kuleta mapungufu ya kinga mwilini saratani,HIV/AIDS,
  • Watu wanaotumia baadhi ya dawa kwa muda mrefu kama steroids

Shukrani
http://www.cdc.gov/flu/about/season/


Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko