Habari kutoka kituo cha kudhibiti magojwa nchini Marekani “Center for Disease Control” ( CDC) 2014 -2015, inatufahamisha kuhusu kipindi cha mafua makali ( Severe FLU Season).
Kipindi hiki kilichotawaliwa zaidi na virusi vya A H3N2,hujulikana kwa kuleta homa kali, ongezeko la wagojwa mahospitalini na hata vifo. CDC inatukumbushia umuhimu wa kila mmoja kupata Chanjo ya Flu na tiba ya haraka ya kupamba na virusi (Anti-viral drugs treatment) hasa kwa watu walio na kinga hafifu. Anti-viral drugs husemekana kuwa mahiri zaidi kati ya masaa 48 baada ya dalili za flu kujitokeza mwilini .
Mabadiliko ya virusi kimaumbile (genetic) huchangia kupunguza umahiri wa chanjo japo wengi waliofanikiwa kupata chanjo huwa na maambukizi afueni. CDC imeongeza kusema, FLU ya kipindi hiki iliyotawaliwa na Influenza A H3N2 ilitokea miaka ya 2012-1213, 2007-2008 na 2003-2004 vipindi ambavyo viliongoza kwa idadi ya vifo katika ya miaka 10 iliyopita.
NINI DALILI ZA FLU
- Kukohoa au kukwaruza kwa koo
- Maumivu ya kichwa
- Baridi
- Kuumwa mwili au uchovu wa mwili
- homa
- Mafua ya maji au yenye kubana
NANI YUU HATARINI
- Watoto chini ya umri wa miaka 5, wazee kuanzia miaka 65
- Asthma
- Wejawazito
- Wagojwa ya Kisukari, Figo,Ini,Circle cell
- Magojwa yenye kuleta mapungufu ya kinga mwilini saratani,HIV/AIDS,
- Watu wanaotumia baadhi ya dawa kwa muda mrefu kama steroids
Shukrani
http://www.cdc.gov/flu/about/season/
Comments
Post a Comment