Skip to main content

PATA PRESCRIPTION MEDICATION KWA BEI NAFUU!


Bofya:
Jina kamili la dawa 
Zip code
Chagua Milgram na Idadi ya  dawa kifuatia agizo la daktari 
Print coupon
Wasilisha katika pharmacy ya anwani  husika

FUATA HATUA SAHIHI ZA  UTUMIAJI  WA DAWA
  • DAWA SAHIHI;
 Dawa huweza kuwa na majina yanayokaribiana hivyo kuwa mwangalifu na kusoma kila mara

  • DOZI SAHIHI;
Vifo vingi husababishwa na utumiaji wa dawa kwa kiwango kisicho sahihi.

  • NJIA SAHIHI
Ili kuepuka madhara, hakikisha unafuata njia sahihi katika matumizi ya dawa mfano dawa ya kumeza, kupaka au kuchoma sindano itumike ilivyokuwudiwa.

ZINGATIA VIPENGELE VIFWATAVYO;
  • Dawa ya kumeza isiyoruhusiwa kutafunwa au kuvunjwa, 
  • Dawa inayotakiwa kutafunwa
  • Dawa inayohitaji kutumiwa na chakula
  • Dawa inayohitaji kutumiwa na kiwango kikubwa cha maji
  • Dawa inayohitaji kutumiwa kwa muda maalum kabla au baada ya chakula 
  • Dawa, vyakula au viywaji vya kuepuka wakati wa matumizi ya dawa husika
  • Kabla ya matumizi ya dawa yeyote mfahamishe daktari wako dawa ambazo unatumia
  • Mfahamishe daktari na nesi kuhusu tatizo lolote la  allergy
  • Ripoti dalili zozote baadaya matumizi ya dawa mpya ikiwemo;kuwashwa, vipele,kuvimbe etc.
  • Soma na uliza maswali kuhusu dawa uliyoandikiwa kabla ya kutumia



  • MUDA SAHIHI
Ili dawa ifanye kazi inavyotakiwa ni vyema kutumika kwa muda uliopangwa, mfano dawa za maumivu endapo umepangiwa kila baada ya masaa manne hadi sita, ukapitiliza maumivu hurudi na huwa magumu zaidi kuyatuliza.

                                                                   


  • KUMBUKUMBU
Baadhi ya makosa katika matumizi ya dawa ni usahaulifu. Mara nyingi usahaulifu utokea pale mtu anapotumia dawa, kisha anasahau kuwa ameshatumia na hivyo  kurudia matumizi na kuzidisha dozi aliyopangiwa. Tatizo lingine  ni kwa WAZAZI  KUTOWASILIANA ; mzazi anaweza  kutoa dawa kwa mtoto na kusahau kumtaarifu mzazi mwenzake. Bila kuwa na mfumo wa kufahamishana, mzazi mwingine anarudia utoaji wa dawa na kuhatarisha uhai.  Hivyo yashauriwa kutumia nyezo za kusaidia usahihi wa matumizi ya dawa kama pills kit, calendar, diary etc.





































Images;
www.halifaxexaminer.ca
askabiologist.asu.edu

http://www.ruanemedical.com/
http://www.ebay.co.uk/

Comments

Popular posts from this blog

HUDUMA YA HARAKA KWA UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI (HYPOGLYCEMIA)

0 Ubongo wa binadamu unahitaji sukari kwa mda wote ili kuwa na nguvu ya kufanya kazi . Sukari hii yategemewa kutoka kwenye mzunguko wa damu kwani ubongo hauna uwezo wa kuzalisha au kuhifadhi sukari ya kutosha  matumizi ya  baadaye. Kutokana na hitilafu ya kingosho(dysfunctional pancreas) wagowja wa kisukari huwa na hali ngumu ya kuweka sukari katika vipimo vinavyohitajikana hivyo mara nyingi  sukari huwa juu (Hyperglycemia) au chini  (Hypoglycemia) na huhitaji tiba. Hivyo basi ni muhimu sana kwa ndugu au rafiki wa karibu kujua machache ili kuwa msaada pale mpendwa wako anapojikuta katika hali ya kuishiwa sukari kwani  inahitaji huduma ya haraka kuokoa maisha. DALILI ZA UPUNGIFU WA SUKARI MWILINI (Hypoglycemia) Kipimo cha sukari  chini ya    70 mg/dL au 3.9 mmol/L   chaweza hatarisha maisha ya mpendwa wako  mwenye kisukari. ; Njaa kuumwa kwa kichwa Kutokwa kwa jasho kutikisika kwa mwili Hasira Mwili au ngozi baridi na nyevu K

UPUNGUFU WA POTASSIUM MWILINI, WAWEZA KUWA TISHIO KWA USALAMA WA MOYO !.

NDIZI HUSIFIKA KWA UTAJIRI WAKE WA MADINI YA POTASSIUM Potassium ni moja  kati  ya madini muhimu ya chumvi chumvi mwilini.Ikisaidiana na chumvu chumvi nyingine kama Calcium, Magnesium na Sodium. Potassium ni muhimu sana kwenye usimamiaji wa kiwango sahihi cha maji mwilini, utendaji wa cell na kikubwa zaidi  uanzishaji wa mwendo ( conduction of  electricity) katika  misuli ya mwili yenye mwendo hiari na mwendo usio wa hiari. Hivyo, hupelekea mwamko katika mishipa ya moyo inayohusika na huwa ndio chanzo cha mapigo yanahusika na msukumo wa  damu mwilini. ( generates heart bit) Mahitaji ya Potassium kwa mtu mzima ni kati ya milligram zisizopungua 3,500 ml. kwa siku kutoka kwenye lishe. Ili mwili wa binadamu uweze kuendelea na utendaji wake, potassium iliyoko katika mzunguko wa damu yahitaji kuwa kati ya 3.5-5.0mEg/L. Kiwango hiki kikipopunguwa hutupelekea hali ijulikanayo kama; Hypokalemia au Upungufu wa Potassium katika damu. Vile vile kiwango hiki kinapozidia huitwa H

MATATIZO YA THYROID KWA WANAWAKE .

Thyroid ni mojawapo ya tezi zilizo mwilini zinazozalisha  homoni  (hormones) zake ndani ya mwili  na kutumika  kwenye mfumo wa  damu. Miongoni mwa kazi za homoni ya thyroid ni    kusimamia  utendaji wa shughuli  mwilini kama mwendo wa mapigo ya moyo,( heart rate),  usagaji wa chakula (digestion) ,mwendo na utendaji wa metaboli (metabolism)  na kusimamia matumizi ya calorie mwilini. Ili tezi ya thyroid iweze kufanya kazi yake ya uzalishaji homoni  huitaji madini ya Iodine.Madini  hayo hupatikana katika vyakula vya mimea vilivyotoka  kwenye udongo wenye virutubisho vya iodine ya kutosha, chumvi yenye iodine na vyakula vya baharini. Tezi ya thyroid inapozalisha homoni pungufu na kipimo kinachohitajika  husababisha  hali ijulikanayo kama   “Hypothyrodism”. Tezi hii  ikizalisha  homoni kupita kipimo kinachohitajika mwilini huitwa “Hyperthyrodism” LEO NINAPENDA KUZUNGUMZA NANYI KUHUSU UGONJWA WA HYPOTHYRODISM Hypothyrodism ni ugojwa ambao huwapata  wanawake zaidi kuliko